Baada ya kurejea nchini, beki Lameck Lawi amesema hatma ya yeye kuitumikia Coastal Union ipo chini ya Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) baada ya Simba kuendelea kukomaa.
Lawi ambaye alisaini mkataba ndani ya Simba, ameshindwa kuitumikia timu hiyo na badala yake alitimkia Ubelgiji kwa ajili ya kujaribu kwenye klabu ya K.A.A Gent lakini mambo yameenda tofauti, hivyo amerudi Tanzania
Lawi akizungumzia namna mchakato wake wa usajili ulivyoenda amesema anapitia wakati mgumu sasa kutokana na kukosa nafasi ya kucheza kuendeleza alipoishia msimu uliopita na hatimaye kufikia malengo.