Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo August 03, 2024
Pitia kurasa za mbele za magazeti ya Tanzania Kitaifa na kurasa za kimichezo, pamoja na gazeti la Michezo ya leo Jumamosi August 03, 2024 na ujipatie nakala yako kwa undani wa habari.
Pitia kurasa za mbele za magazeti ya Tanzania Kitaifa na kurasa za kimichezo, pamoja na gazeti la Michezo ya leo Jumamosi August 03, 2024 na ujipatie nakala yako kwa undani wa habari.
Maelfu wamejitokeza kuhudhuria mazishi ya kiongozi wa kisiasa wa Hamas, Ismail Haniyeh, nchini Iran ambaye aliuawa katika shambulizi mjini Tehran siku ya Jumatano. Kiongozi Mkuu wa Iran, Ayatollah Ali Khamenei, anaongoza sala hiyo kabla ya kiongozi huyo kuzikwa nchini Qatar. Vyombo vya habari vya Marekani vimewanukuu maafisa wa Iran wakisema kiongozi huyo mkuu ameamuru shambulio…
‘Bundi’ wa majeraha ameendelea kuiandama klabu ya Manchester United baada ya juzi beki wao mpya Leny Yoro kuumia kwenye mchezo wa maandalizi ya msimu dhidi ya Arsenal na kusadikika kuwa nje ya uwanja kwa karibu miezi miwili, leo tena alfajiri washambuliaji wao wawili Marcus Rashford na Antony kuumia na kushindwa kumaliza mchezo kwenye mchezo wa…
Usiku wa tarehe 1 August 2024, katika jiji la Dar Es Salaam limefanyika moja kati ya tukio kubwa la kimichezo katika nchi ya Tanzania, nalo ni ugawaji wa tuzo kwa wachezaji waliofanya vyema katika msimu wa 2023/2024, Tuzo zinazofahamika kama TFF Awards ambapo zimefanyika katika ukumbi wa Super Dome. Katika Usiku Huo wa ugawaji wa…
Jeshi la Israel limethibitisha lilimuua mkuu wa kijeshi wa kundi la wapiganaji wa Hamas, Mohammed Deif, katika shambulio lililotumia ndege za kivita katika eneo la Khan Yunis tarehe 13 ya mwezi Julai. Madai ya Israeli kumuua Deif yamekuja ikiwa imepita siku moja baada ya kuuawa kwa kiongozi mkuu wa Hamas Ismail Haniyeh mjini Tehran. Israeli…
Maelfu ya wananchi Nchini Nigeria wamejitokeza katika maeneo mbalimbali kufanya maandamano ya amani waliyopanga kuyaanza leo Agosti 1 hadi 10 2024 wakipinga mfumuko wa bei kama chakula,maji, mavazi na utawala mbaya wa Rais wao Bola Ahmed Tinubu. Katika maandamano hayo yanayoendelea hii leo baadhi ya waandamanaji wamechoma moto jengo la hifadhi ya viwanda vya kidigitali…
Video ya ngoma ya Jeje ya msanii Diamond Platnumz imefikisha watazamaji milioni 100 kwenye mtandao wa YouTube na kuwa video ya kwanza ya msanii huyo aliyoimba pekee yake kufikisha watazamaji milioni 100 Youtube akiwa msanii wa pili Tanzania na Afrika Mashariki. Hivi karibuni video ya wimbo wa Sukari (2021) ya msanii Zuchu uliweka rekodi ya…
Pitia kurasa za mbele za magazeti ya Tanzania kitaifa na kurasa za kimichezo pamoja na gazeti la Michezo ya leo Ijumaa August 02, 2024 na ujipatie nakala yako kwa undani wa habari.