Messi ndio aliyebarikiwa baada ya kumgusa Lamine

Mounir Nasraoui [ Baba mzazi wa Lamine ] ameteka vichwa vya habari baada ya kusema Messi kumgusa Yamal utotoni sio kama alimbariki badala yake Messi ndiye aliyepata baraka za Yamal.

 

“Messi amembariki Lamine? Labda Messi ndiye aliyebarikiwa baada ya kumgusa Lamine Yamal [akacheka]”.

 

“Lamine alikomaa kabla ya wengine, ninawashukuru sana Hispania ,La Masia, marafiki na wengine wote”.

 

Inawezekana Baba mzazi wa Lamine akawa na hoja kwa sababu , Messi kabla ya kumgusa Yamal alikuwa na magoli chini ya 30 katika misimu yake mitatu ya kwanza akiwa na Barcelona , baada ya kumgusa Yamal kila mtu anajua mambo makubwa yaliyofanywa na Messi kwenye mpira wa miguu.

One thought on “Messi ndio aliyebarikiwa baada ya kumgusa Lamine

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *