Mzambia Mwingine Aipa ‘ Thank You’ Simba Baada Ya Chama

Mshambuliaji wa Zambia, Moses Phiri ameaga rasmi na kuthibitisha kuwa hatakuwa sehemu ya kikosi cha Simba kwa msimu ujao ikiwa ni wiki kadhaa baada ya Mzambia mwenzake Clatous Chama kuondoka msimbazi na kujiunga na Yanga.

“Leo ndio siku ya mwisho mimi kuwa mchezaji wa Simba, shukrani zote ziwaendee wachezaji nilioshirikiana nao, viongozi wa Simba na Rais Mo Dewji kwa kunifanya kuwa sehemu ya historia ya Simba Ahsante sana.”

“Mwisho kwa mashabiki wote wa Simba, Nawapenda sana asanteni kwa upendo na ushirikiano mlionipa, daima mtabaki moyoni mwangu, tutakutana Tena mjini hapo bongo nikija kufanya biashara” — Moses Phiri

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *